MALORI YA TANZANIA YARUHUSIWA KUPITA KWA TOZO YA ZAMANI MPKANI RWANDA
 Naibu  Waziri wa Uchukuzi  Dk. Tzeba  amethibitisha kuwa Serikali ya Rwanda  imeruhusu malori ya Tanzania yaendelee na safari kwa kulipa dola 152  badala ya 500 zilizoanza kutozwa hapo  jana.
 Akiongea   toka  mkoani  Dodoma, Tzeba  ameweka  wazi  kuwa  Waziri wa Fedha wa  Rwanda  aitwaye Gatete na wa  waziri  wa  Uchukuzi wa  Rwanda aitwaye   Rwakabamba, wameridhia tozo ya dola 152  iendelee  kutumika.
Tzeba  amedai  kuwa  ofisa mmoja katika Wizara ya Fedha ya Rwanda ndiye aliyekurupuka na  kutangaza mabadiliko hayo kwa mdomo.
Waziri  wa Fedha wa Rwanda alipoulizwa  na mwenzake wa Tanzania, alishituka  na kuahidi kulipatia ufumbuzi   tatizo  hilo ambapo  ndani ya muda  mfupi  jibu lilipatikana kuwa agizo  la  ofisa huyo wa Rwanda halikuwa halali. 
Mbali  na  kauli  ya  Tzeba, habari  za  CHUMBANI  ambazo  mpekuzi  wetu   amezipata  zinadai  kwamba  uamuzi huu  umefikiwa  na  serikali  ya  Kagame  baada ya Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA)  kulazimika kupunguza  ushuru wa barabara ( Road Toll) kwa magari yenye  plate numbers za  Rwanda  kwa  asilimia  170. 
 Kwa  hali  hii, ni  dhahiri  kuwa  huu  utakuwa  ni ushindi mkubwa kwa Rwanda ikizingatiwa kuwa  umbali kutoka  Dar  es Salaam mpaka Rusumo ( mpakani )sio sawa na umbali kutoka Rusumo mpaka  Kigali.
 
 
 
          
      
 
   
  
 
0 komentar:
Post a Comment